habari

MATANGAO

Friday, November 23, 2012


MAMBO yameiva Yanga- matumaini ya wapenzi wa klabu hiyo kushuhudia klabu yao ikiwa na Uwanja mpya wa kisasa yameanza kuonyesha dalili za kutimia, kufuatia uongozi wa klabu hiyo kusaini makubaliano ya awali na Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group iliyojenga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Kaunda.Mwenyekiti wa mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati, Alhaj Yussuf Mehboob Manji leo amesaini makubaliano na Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo, David Zhang, makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Jangwani na Twiga, Dar es Salaam.Katika makubaliano hayo, ujenzi huo wa Uwanja utakaokuwa na uwezo wa kuchukua mashabiki 30,000 hadi 40,000 utaanza rasmi Juni mwakani.Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa kusaini makubaliano hayo leo mchana, Alhaj Manji alisema kwamba wanfurahi kuanza safari ya ujenzi wa Uwanja wao na anaamini huo ni mwanzo wa mzuri wa mipango yao ya kuifanya Yanga ijitegemee kiuchumi.Katika hatua nyingine, Manji amesema kwamba katika mipango yao ya kuifanya Yanga ijimudu kiuchumi, wanafikiria kulikarabati pia jengo dogo la klabu hiyo, liliopo Mtaa wa Mafia.Alhaj Manji alisema Jumatatu kampuni hiyo ya ujenzi kutoka China, ambayo ndiyo iliyojenga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itachukua vipimo kwenye Uwanja wa Kaunda na Uongozi wa Yanga kuliwasilisha suala la ujenzi huo kwenye Mkutano Mkuu wa Wanachama wa klabu hiyo, Desemba 8, mwaka huu.Alisema baadhi ya fedha kwa ajili ya uwanja huo wa kisasa watakapo benki na gharama nyingine zitatokana na michango ya wanachama baada ya kuwa wamepata gharama nzima za ujenzi za uwanja huo.Meneja Mkuu wa Kampuni ya Beijing Cobnstruction Engineering Group alisema wanafurahia kufikia makubaliano ya awali ya ujenzi wa uwanja na klabu ya Yanga.Alisema wao ndio walijenga Uwanja wa Taifa na viwango vya ujenzi vya uwanja huo vilisifiwa na timu ya taifa ya Brazil iliyokuja kucheza mechi ya kirafiki na Tanzania mwaka 2010 ikiwa njiani kuelekea Afrika Kusini ambako fainali za kombe la Dunia zilifanyika.

Sunday, November 11, 2012


PICHA ZA SIMBA SPORT CLUB NA TOTO AFRICAN JANA WALIVYOBANWA SIMBA KATIKA UWANJA WA DAR-ES -SALAAM,TOTO AFRICAN WAKI UBUKA NA USHINDI WA 1-0.




YANGA imeendelea kuwapa raha mashabiki wake, baada ya kufanikiwa kumaliza vema mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ikijishindilia kileleni zaidi, kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Coastal Union, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Yanga imemaliza mzunguko wa kwanza ikiwa na pointi 29, ikifuatiwa na Azam FC katika nafasi ya pili yenye pointi 24 na Simba SC nafasi ya tatu kwa pointi zao 23.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0. Lililotiwa kimiani na mshambuliaji wake wa kimataifa wa Burundi, Didier Kavumbangu dakika ya 28, kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na kiungo Simon Msuva.
Kipindi cha pili, Yanga walirejea na moto wao tena na iliwachukua dakika 17 tu kuandika bao la pili, mfungaji Mganda Hamisi Kiiza ‘Diego’ aliyeuwahi mpira ambao aliuokosa beki wa Coastal, Mbwana Hamisi na kuutumbukiza nyavuni kiulaini.
Yanga SC; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Nurdin Bakari, Frank Domayo, Simon Msuva, Hamisi Kiiza, Haruna Niyonzima na Didier Kavumbangu/Said Bahanuzi.
Coastal Union; Juma Mpongo, Ismail Amour Khamis, Juma Jabu, Jamal Macherenga/Othman Omar Tamim, Mbwana Hamisi, Jerry Santo, Soud Mohamed, Razack Khalfan, Daniel Lyanga, Atupele Green/Lameck Dayton na Suleiman Kassim ‘Selembe’.

Friday, November 9, 2012

CHAGUENIKIKOSI KITAKACHO SHINDA MECHI ZA TANZANIA.
SIMBA SPORT CLUB.
YOUNG AFRICAN SPORT CLUB

CHAGUENIKIKOSI KITAKACHO SHINDA MECHI ZA TANZANIA.
AZAM FOOTBALL CLUB
JKT MGAMBO
MTIBWA SUGAR.
COASTAL UNION.

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania .


SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania limeteua wadau 10 kwa ajili ya kusaidia timu ya taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys itakayopambana na Congo (Brazaville) katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika.
Uteuzi huo umefanywa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya Kamati ya Vijana ya TFF kufanya kikao chake kujadili kwa umakini ushiriki wa timu hiyo na kupeleka mapendekezo yake kwa rais huyo wa shirikisho.
Kutokana na umuhimu wa mechi hiyo itakayoamua timu itakayofuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, TFF imeona umuhimu wa kuwa na kamati ambayo itakuwa na majukumu mawili makubwa ambayo ni:
1. Kuhamasisha vijana waone umuhimu na kuwa na ari ya kushinda mechi hiyo
2. Kuhamasisha umma uone umuhimu wa mechi hiyo na hivyo kuisaidia iweze kufuzu.
Walioteuliwa kuunda kamati hiyo ni:1. Ridhiwani Kikwete Mwenyekiti2. Ahmed Seif (Magari) Mjumbe3. Nassoro Bin Slum Mjumbe4. Henry Tandau Katibu5. Ahmed Mgoyi Mjumbe6. Aboubakar Bakhresa Mjumbe7. Angetile Osiah Mjumbe8. Kassim Dewji Mjumbe9. Abdallah Bin Kleb Mjumbe10. Salim Said Mjumbe
Baada ya kuvuka raundi mbili za kwanza bila ya kucheza mechi kutokana na wapinzani wake kujitoa, timu ya Serengeti Boys inahitaji kufanya kila iwezalo kuweza kuiondoa Congo kwenye mashindano hayo na kuweka rekodi ya kufuzu kucheza fainali hizo za Afrika ambazo pia zitatoa wawakilishi wa Afrika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia. 
Mechi za kwanza za raundi ya tatu zitachezwa kati ya Novemba 16 na 18, 2012 na mechi za marudiano zitachezwa kuanzia Novemba 30, 2012 hadi Desemba 2, 2012

Tuesday, November 6, 2012


KIPA wa zamani wa Simba na aliyekuwa kocha wa makipa wa timu hiyo, Iddi Pazi ‘Father’ amesema kwamba uwezo wa kipa namba moja wa sasa klabu hiyo umeshuka na tiba yake anaijua.“Kaseja uwezo umeshuka kidogo, kwa sababu daktari wake sipo pale, Simba wakinirudisha kazini, Kaseja atafufua makali yake na atakuwa hafungiki kwa urahisi,”alisema Pazi.Pazi ameushauri uongozi wa Simba umerejeshe kazini ili aokoe kipaji cha kipa huyo bora, miongoni mwa walinda milango bora kuwahi kutokea Tanzania.Kwa sasa, kocha wa makipa wa Simba ni kipa mwingine wa zamani wa Simba, James Kisaka ambaye alipewa kazi hiyo baada ya Pazi kwenda Oman. Lakini kwa sasa Pazi amemaliza mkataba wake Oman na yupo nyumbani kwake, Majumba Sita, Ukonga, Dar es Salaam.Katika mechi 12, Kaseja amefungwa mabao 10 kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzanoia Bara msimu huu, kitu ambacho si kawaida yake katika misimu iliyotangulia, ingawa hiyo inaelezwa inachangiwa hata na ubutu wa safu ya ulinzi ya sasa wa timu hiyo.Lakini pia, kocha Mserbia wa Simba SC, Profesa Milovan Cirkovick naye anadaiwa kuchangia matokeo mabaya na habari zinasema anaweza kutimuliwa wakati wowote kwenye klabu hiyo, kufuatia kutofautiana na uongozi wa klabu hiyo.Uongozi wa Simba unamtuhumu Mserbia huyo kwamba ni mbishi hashauriki na hilo limekuwa likiigharimu timu katika michezo yake ya karibuni ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.“Huyu jamaa tumemvumilia sana, mimi sina hamu naye tena, sijui wenzangu. Anapanga kikosi ovyo na ndiyo chanzo cha matokeo haya mabaya,”alisema kiongozi mmoja wa Simba. Lakini kwa upande mwingine, inadaiwa matokeo haya mabaya ya Simba ni matokeo ya mgomo wa wachezaji wakishinikiza wachezaji wenzao waliosimamishwa Haruna Moshi ‘Boban’ na Juma Nyosso warejeshwe kikosini.Zaidi Boban, wachezaji wanadaiwa kumpenda sana kutokana na roho yake safi ya kibinadamu na upendo mkubwa kwa wenzake.Boban ndiye mchezaji pekee aliyejitolea kuusindikiza nyumbani kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) mwili wa marehemu Patrick Muteesa Mafisango, kiungo wa Simba aliyefariki dunia Mei mwaka huu kwa ajali ya gari.Simba SC juzi ilifungwa mechi ya kwanza ya Ligi Kuu mabao 2-0 na Mtibwa Sugar, Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, mabao ya Said Mkopo na Hussein Javu.Simba inabaki na pointi zake 23, baada ya kucheza mechi 12, ikiipisha kileleni Yanga yenye pointi 26 sasa. Simba itamaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kwa kumenyana 

Sunday, November 4, 2012



YANGA SC imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuifunga Azam FC mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga iongoze Ligi Kuu kwa kufikisha pointi 26, ikiwa imebakiza mechi moja ya mzunguko wa kwanza dhidi ya Caostal Union mjini Tanga, ikifuatiwa na Simba SC yenye pointi 23, ambayo leo imefungwa 2-0 na Mtibwa Sugar mjini Morogoro.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Didier Kvumbangu aliyeunganisha krosi ya Simon Msuva kutoka wingi ya kulia dakika ya tisa.
Katika kipindi hicho, Yanga timu zote zilicheza kwa kiwango sawa, isipokuwa Yanga ndiyo iliyokuwa na mashambulizi ya kutisha zaidi.
Mabeki wa Yanga walimdhibiti vema mshambuliaji hatari wa Azam, John Bocco ‘Adebayor’ na kitendo cha kocha Mholanzi, Ernie Brandts kupanga viungo wawili wakabaji, Athumani Iddi ‘Chuji’ na Frank Domayo viliisaidia timu hiyo kuwabana Azam  katikati ya Uwanja.
Kipindi cha pili, Yanga walirudi vizuri zaidi na kuifunika kabisa Azam, ambayo leo hakika ilimsononesha kocha wake, Muingereza Stewart Hall.
Mganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ aliifungia Yanga bao la pili dakika ya 68, akiunganisha krosi ya Athumani Iddi ‘Chuji’ kutoka wingi ya kulia.
Baada ya bao hilo, Kiiza alivua jezi yake na kubaki na fulana ya njano yenye maandishi; Rest In Peace Mafisango, I miss you So much my brother, maana yake akimuenzi aliyekuwa kiungo wa Simba, Patrick Mutesa Mafisango aliyefariki dunia kwa ajali ya gari Mei mwaka huu akiwa mchezaji wa klabu hiyo.
Kwa ujumla Yanga imebadilika mno kiuchezaji na sasa wanacheza kwa kuonana, kupeana pasi za uhakika ndefu na fupi, kuwabana wapinzani na pia bila kuchoka muda wa mchezo.
Kikosi cha Yanga SC leo kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Frank Domayo, Simon Msuva/Paul Ngalema, Hamisi Kiiza, Haruna Niyonzima na Didier Kavumbangu.
Azam FC; Mwadini Ally, Erasto Nyoni/Samir Hajji Nuhu, Ibrahim Shikanda, Aggrey Morris na Said Mourad, Jabir Aziz/Ibrahim Mwaipopo, Kipre Balou, Khamis Mcha ‘Vialli’/Abdi Kassim ‘Babbi’, Salum Abubakar, John Bocco na  Kipre Tcheche.
Katika mchezo wa utangulizi, Yanga B imewafunga Azam B, maarufu kama Azam Academy mabao 2-0. Mabao ya Yanga B yalifungwa na Joseph Banda na Claver Charles kipindi cha kwanza.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo, Mtibwa Sugar iliichapa mabao 2-0 Simba SC, Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, mabao ya Said Mkopo na Hussein Javu.
Simba inabaki na pointi zake 23, baada ya kucheza mechi 12, ikiipisha kileleni Yanga yenye pointi 26 sasa. Simba itamaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kwa kumenyana na Toto African uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.